MADHARA YA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA TIBA YAKE Upungufu wa Nguvu za Kiume ni hali ya kushindwa kufanya mapenzi kikamililifu au kushindwa kusimamisha vizuri, shughuli ya tendo la ndoa huhusisha akili, homoni, neva, misuli, hisia na mirija ya damu. Tatizo hili huripotiwa kuwa katika wanaume watano (5) basi mmoja kati yao anatatizo la upungufu wa nguvu za kiume. Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kuto kuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalohitaji tiba. CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME Tatizo la nguvu za kiume lina vyanzo vingi ambavyo mara nyingi wengi huvipuuza, hivyo vyanzo huathiri taratibu na vingine huathiri haraka, tunashauri watu kuwa makini sana ili kujiimarisha vizuri. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata tatizo la nguvu za kiume nayo ni pamoja na; 1.Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P) au ugonjwa wa moyo 2.Kuvuta sigala na unywaji wa pombe 3.Uzito kupita kiasi na unene uliozidi 4.Ulaji ho...